Kwa sababu tumeshaeleza mambo yaliyotokea katika safari yetu katika insha zetu, nilidhani kwamba ni mwafaka kuanzia mada tofauti. Ningetaka tuzungumzie matatizo yanayokabili dunia yetu kuhusu ukosefu na bei ghali za chakula, ambazo zinatatiza watu wengi kote duniani. Kila siku vyombo vya habari vinaripoti kuhusu maandamano yanayoendelea katika nchi kadha wa kadha kuhusu matatizo haya, na kwamba watu maskini milioni kadhaa hawawezi kujilisha. Kwa mfano, bei ya mchele, ambao ni chakula kikuu cha watu wengi duniani, imepandia asilimia tisini katika mwaka mmoja uliopita.
Nilisoma tu leo kuwa Katiba Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bw. Ban Ki-Moon, baada ya mikutano anajitayarisha kutangaza mipango ya kujaribu kukabili shida zinazosababishwa na ongozeko la bei za chakula. Je, sababu zipi zimesababisha shida hii? Unafikiri mipango ambayo itatangazwa itasaidia vipi? Unadhani kuna sera ambazo zitaweza kufumbua (solve) matatizo haya na labda matatizo haya yametukia kwa upande kwa sababu hatuna uwezo wa kulisha idadi ya watu wanaoishi duniani leo?
Monday, April 28, 2008
Sunday, April 6, 2008
Kufuzu kwa Daudi Kwenda Olimpiki na Safari yenu ya Wingereza
Habari za leo? Nitaanza mfululizo wetu wa mada za blogu kwa muhula huu. Naanza kwa kumpongeza Daudi kwa dhati kwa kufaulu kujiunga na timu ya Kenya kwenda kwa michezo ya olimpiki mwaka huu. Pongezi.
Ningependa mkipata nafasi mtoe maelezo kuhusu safari yenu kwenda Wingereza pamoja na namna mashindano yenu yanavyoendelea. Aidha, nawatakia kila la heri huko.
Kwaherini.
Ningependa mkipata nafasi mtoe maelezo kuhusu safari yenu kwenda Wingereza pamoja na namna mashindano yenu yanavyoendelea. Aidha, nawatakia kila la heri huko.
Kwaherini.
Subscribe to:
Posts (Atom)