Ningetaka kuanza mazungumzo mafupi kuhusu riwaya ya 'Rosa Mistika' tunayosoma wakati huu. Tumeona sifa za Rosa zikibadilika na tabia zake kuzorota na Kezilahabi anasema ni kwa sababu ya malezi yake. Je, katika maisha halisi unafikiri kwamba malezi yangeweza kusababisha sifa za mtu kubadilika upesiupesi kama jinsi sifa za Rosa zimebadilika? Je, kuhusu mbinu ya Padri kumzungumzia Rosa, ulifikiri mbinu zake zilikuwa mwafaka? Ungekuwa katika msimamo wake ungesema nini kujaribu kumsaidia Rosa? Unadhani kuna imani yo yote kwa Rosa?
Katika riwaya hii tunakabiliwa na swala la kutoa mimba na tunaona mawazo tofauti kuhusu swala hili. Je, maoni yako kuhusu swala hili ni nini? Unadhani mawazo ya Regina yangekuwa kuhusu swala hili yangekuwa tofauti iwapo angezaa wavulana tu?
Thursday, February 21, 2008
Sunday, February 10, 2008
Mipango ya maisha yenu ya baadaye
Habari za leo?
Baada ya mjadala kuhusu hali ya kisiasa nchini Kenya pamoja na umuhimu na ongezeko la athari za Uchina ulimwenguni, nataka tugeukie swala tofauti linalohusiana na maisha yetu. Mimi napanga kurudi Kenya na kutoa mchango wamgu katika kufundisha. Aidha, nadhani nitafurahi mno ikiwa nitawza kuanzisha shule ya kuwasaidia vijana chipukizi kupata elimu nzuri. Tayari mimi nina mke na mtoto mmoja na napanga kupata wengine. Ningependa kujua mipango yenu ya baadaye maishani (baada ya Stanford). Zingatieni maswala kama masomo, kazi, familia, sehemu ya kuishi na kadhalika.
Baada ya mjadala kuhusu hali ya kisiasa nchini Kenya pamoja na umuhimu na ongezeko la athari za Uchina ulimwenguni, nataka tugeukie swala tofauti linalohusiana na maisha yetu. Mimi napanga kurudi Kenya na kutoa mchango wamgu katika kufundisha. Aidha, nadhani nitafurahi mno ikiwa nitawza kuanzisha shule ya kuwasaidia vijana chipukizi kupata elimu nzuri. Tayari mimi nina mke na mtoto mmoja na napanga kupata wengine. Ningependa kujua mipango yenu ya baadaye maishani (baada ya Stanford). Zingatieni maswala kama masomo, kazi, familia, sehemu ya kuishi na kadhalika.
Monday, February 4, 2008
Mnataka mwe nini wakati ujao? (kutoka kwa Upendo)
Mnataka mwe nini wakati ujao?Hamjambo wote! Habari za wikendi? Nilifikiria kuhusu ninyi wikendi hii, na nilitanabahi nisijue nini mnataka mwe wakati ujao. Mimi, ningependa kuandika au kuumba sera ya afya kimataifa. Msiulize - sitaki kuwa dakta. Ningependa kuwa mwanasheria ambaye anajua mambo mengi kuhusu sheria ya dunia na ya haki za watu. Kwa hivyo, nilisoma historia mpaka mwaka huu, na sasa, ninasoma elimu jamii (hasa kuhusu siasa linganishi) ili nifahamu hali ya dunia nzima.Na nyi? Mnataka kuwa nini wakati ujao? Na kwa nini?Tutaonana kesho! ~Upendo
Subscribe to:
Posts (Atom)