Saturday, January 26, 2008

Umuhimu wa Uchina

Ingawa mauaji yanaendelea katika nchi yetu na hawajasuluhisha cho chote, nilifikiri kuwa nitatoa mazungumzo yetu kwa mkondo na kuwauliza maswali machache kuhusu Uchina. Juzi katika chajio nilikuwa nikzungumza na rafiki zangu kuhusu lugha za Uchina na umuhimu wao. Kulikuwa na wale ambao walinena kwamba katika siku za usoni itakuwa muhimu zaidi kuelewa lugha hizo kwa sababu angalau asilimia ishirni ya umma wa dunia wanatoka Uchina. Kwa hivyo swali langu ni: Je, unadhani kwamba ni muhimu kujifunza lugha hizo hata usipotaki kwenda kuishi nchini Uchina?

Swala langu la pili ni kuhusu upanuzi wa Uchina. Uchumi wake umekuwa ukikua kwa miaka thelathini tangu serikali iliongoa shughuli za nchi. Kuna sababu nyingi kuhusu maendeleo ya uchumi wake lakini watu hutaja kwamba Wachina hawajali haki za binadamu na kwa hivyo wanaweza kufanya cho chote ili watengeneze pesa. Mfano maarufu ya hii ni kuwa Uchina wanashirikiana kwa shingo upande mjini Darfur. Kwa hivyo, swali langu ni: Je, unafikiri kwamba nchi za kimagharibi wana haki za kujiingiliza shughuli za Wachina ili wasimamishe matukano ya haki za binadamu yanayoendelea nchini Uchina na aidha katika sehemu nyingine duniani? Kulikuwa wazo la kugoma olympiki mwaka huu kwa sababu ya dhima ya Uchina nchini Sudan, unadhani kwamba wazo lingebadilisha kitu?

Friday, January 18, 2008

Maandamano nchini Kenya

Wiki ningetaka kuendelea na mazungumzo yetu ya wiki iliyopita kuhusu matatizo yanayoendelea Kenya. Kwa siku tatu sasa, washabiki wa wapinzani wamekuwa wakiandamana dhidi ya matokeo ya uchaguzi baada ya matangazo ya viongozi wa ODM wiki iliyopita kufanya hivyo. Taarifa za habari zimeripoti kwamba watu zaidi ya kumi wameuawa na wengi wameshtaki polisi kwa vitendo yao. Kwa hivyo swali langu la kwanza ni je, unadhani kwamba polisi wamefanya kazi mbaya wakijaribu kusimamisha maandamano? Ikiwa hawangejiingiliza (interfere), hali ingekuwa heri kuilko sasa?

Juu ya hayo, Annan yuko karibu kufika Kenya kwa ziara yake na atazungumza na Raila na Kibaki ili ajaribu kupata amani. Iwapo ungekuwa Annan ungewaambiaje viongozi hawa? Mpango wako kujaribu kutafuta suluhisho ili Kenya irudie hali ya kawaida ungekuwa nini?

Hatimaye, wapinzani wametangaza watagoma (boycott) mashirika mbalimbali yanayommilikiwa na wenza Wakikuyu wa Kibaki. Je unadhani kwamba kitendo hiki kitakuwa na manufaa kuhusu utafutaji wa suluhisho?

Saturday, January 12, 2008

Uchaguzi wa Urais Nchini Kenya

Habari za wikendi?

Hali iliyoibuka nchini Kenya baada ya uchaguzi wa mwezi jana ilikuwa kinyume kabisa na matarajio ya watu wengi. Kwa maoni yako, hali hii inaweza kuwa na athari gani kwa taifa? Je, unadhani ingeweza kuepukika? Hatua gani zaweza kuchukuliwa kutoa suluhisho?

Jioni njema.